• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Sekta ya kahawa kuboreshwa nchini Kenya

    (GMT+08:00) 2020-04-22 19:55:14
    Wizara ya Kilimo nchini Kenya imeanzisha mpango wa kufufua sekta ya kahawa wa shilingi bilioni 1.5 bilioni ambao utanufaisha kaunti nane zinazozalisha asilimia 70 ya kahawa.

    Akizindua mpango huo waziri wa kilimo Peter Munya alisema lengo la serikali ni kuboresha uzalishaji na ubora wa kahawa nchini humo ambayo imekuwa ikipungua kwa kasi.

    Programu hiyo itafadhiliwa na mkopo kutoka Benki ya Dunia na baadaye inatarajiwa kufikishwa kwenye maeneo yote yanayokuza kahawa.

    Awamu ya kwanza ya mradi huo itawalenga wakulima wa kaunti za Machakos, Kiambu, Muranga, Kirinyaga, Nyeri, Embu, Meru na Tharaka Nithi.

    Uzalishaji wa kahawa nchini Kenya kwa sasa ni tani 40,000 na serikali inatarajia kuongeza uzalishaji hadi tani 100,000 kila mwaka.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako