Rais John Magufuli amewataka waajiri wote wa serikali na sekta binafsi kutotumia mlipuko wa virusi vya corona kama kigezo cha kuwanyanyasa wafanyikazi wao.
Rais anasisitiza kwamba serikali yake inafahamu umuhiu walio nao wafanyikazi wote katika ujenzi wa taifa. Kwenye taarifa hiyo ya kuadhimisha sherehe za leba za mwaka huu, rais alitilia mkazo hatua ya serikali yake kuendelea kusimamia maslahi ya wafanyikazi na kuboresha mazingira yao ya kazi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |