• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Benki ya Kimataifa ya Biashara (CIB), imemaliza kununua Benki ya Kenya Mayfair Bank Ltd (MBL).

    (GMT+08:00) 2020-05-05 19:37:15

    Benki ya Kimataifa ya Biashara (CIB), sekta kubwa ya kibinafsi ya wakopeshaji wa Misri, inalenga ununuzi zaidi Afrika Mashariki baada ya kumaliza kununua Benki ya Kenya Mayfair Bank Ltd (MBL).

    CIB imeorodheshwa kwenye soko la hisa la Wamisri na London, na inajivunia msingi wa mali zaidi ya $ 24 bilioni.

    Mkopeshaji Mmisri alipata hisa nyingi (asilimia 51) katika Benki ya Mayfair ya Kenya kwa mtaji wa dola milioni 35.

    Mnamo Aprili 24, Benki Kuu ya Kenya ilitangaza kumalizika kwa mpango wa CIB-Mayfair, baada ya kupitisha shughuli pesa Aprili 7.

    Mkopeshaji wa misri analenga watu binafsi, wafanyabiashara wadogo na wa kati (SMEs), taasisi na mashirika.

    mwenyekiti wa Mayfair Anjay Patel katika taarif amesema Ushirikiano wa Benki ya Mayfair-CIB unatarajiwa kufaidi wateja na kupanua biashara kati ya Kenya na Misiri.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako