Ripoti ya kila wiki ya Google kuhusu usafiri wa watu umeonesha kuwa wakenya wameanza kurejea kazini.
Ripoti hiyo imeonesha kuwa asilimia 16 ya wakenya walirejea kwenye kazi zao wiki iliopita.
Mkuu wa mawasiliano wa Google barani Afrika Dorothy Ooko amesema hata hivyo watu wanaoondoka nyumbani kwao kila siku kwenda kazini wamepungua kutoka asilimia 25 hadi 20.
Watu pia wamepungua kwa asilimia 5 kwenye mikahawa, maduka na kumbi za sinema.
Kampuni hiyo inatumia teknolojia ya Google Maps kukusanya data kuhusu usafiri wa watu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |