Winga wa kimataifa wa Algeria Farid El Melali, 22, anayeichezea klabu ya Angers ya Ufaransa ameingia kwenye kashfa nzito baada ya kushitakiwa kwa kujichua hadharani. Siku ya Jumatatu El Melali alipewa mkataba mpya wa kuitumikia Angers hadi 2023. Angers ni miongoni mwa klabu shiriki za Ligi Kuu Ufaransa ( Ligue 1). Katika utetezi alioutoa Farid El Melali anasema kuwa hakujua wakati anafanya tukio hilo kama kulikuwa na watu zaidi yake, mwanasheria wake Sandra Chirac-Kollarick anasema mteja wake hakuwa amemlenga mtu yeyote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |