Nyota wa Juventus Paulo Dybala amepona virusi vya corona baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu. Dybala awali alipimwa mara nne corona na kukutwa bado ana maambukizi kitu ambacho alieleza kilikuwa kikimtesa. March 21 Dybala na mpenzi wake Oriana Sabatini waligundulika kuwa na maambukizi hayo kwa mara ya kwanza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |