Uganda inatarajiwa kupokea mkopo wa dharura wa jumla ya dola milioni 491.5 kutoka kwa shirika la fedha la kimataifa IMF kwa ajili ya kukwamua uchumi wake ambao umeathiriwa na janga la Corona. Kwenye taarifa yake, IMF imesema sekta muhimu za uchumi nchini humo ikiwemo sekta ya utalii zimeathiriwa pakubwa na janga la Corona ambalo linaendelea kutikisa dunia hivi sasa. Uchumi wan chi hiyo pia umepata pigo kubwa zaidi kufuatia marufuku ya kutotoka nje kwa raia wote wan chi hiyo kwa ajili ya kuzuia kuenea kwa virusi vya Corona.Nchi ambazo zinapokea mkopo wa dharura kutoka kwa IMF zinatakiwa kulipa mkopo huo ndani ya miaka kumi bila riba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |