• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Uchumi hatarini kuzama

    (GMT+08:00) 2020-05-11 19:01:53
    Wakati huu wa janga la corona, Kenya ni miongoni mwa mataifa yanayoathirika sana kiuchumi.

    Kwa msingi huu, wataalamu wanasema ingehitajika taifa litenge fedha ambazo zingesaidia kufufua uchumi wakati janga la corona litakapoondoka. Badala yake, imebainika fedha nyingi zimetengewa ulipaji madeni kwenye bajeti ya mwaka huu wa kifedha.

    Wataalamu hao sasa wanapendekeza serikali iangalie upya makadirio ya bajeti hiyo ya Sh3.15 trilioni ya mwaka wa kifedha wa 2020/2021.

    Afisi ya Bajeti katika Bunge (PBO) pamoja na Mbunge wa Gatundu Kusini, Bw Moses Kuria, walitambua kwamba katika bajeti hiyo ambayo ndiyo kubwa zaidi kuwahi kuwepo nchini, fedha zilizotengewa masuala ya corona ni Sh2.6 bilioni pekee.

    Hizi si fedha ambazo zitatumiwa kuinua uchumi na kulinda wananchi kiriziki, bali zimenuiwa kutumiwa kupima wananchi kwa wingi ili kubainisha walioambukizwa virusi vya corona.

    Madeni ya Kenya kwa jumla yalipita Sh6 trilioni kufikia mwishoni mwa mwaka wa 2019, kwa mujibu wa takwimu za Benki Kuu ya Kenya (CBK).

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako