Msemaji wa Wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Zhao Lijian amesema, waziri wa mambo ya nje wa China Bw. Wang Yi kesho hapa Beijing atashiriki kwenye Mkutano wa mawaziri wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai SCO utakaofanyika kwa njia ya video.
Bw. Zhao Lijian ameeleza kuwa, katika mkutano huo, mawaziri hao watajadiliana kuhusu ushirikiano katika mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona, hali ya kimataifa na ya kikanda, na maendeleo ya jumuiya hiyo katika kipindi kijacho.
Bw. Zhao anaamini kuwa, pande zote zinazohusika zitaimarisha ushirikiano na kuhimiza jumuiya hiyo kutoa mchango kwa ajili ya ushirikiano wa kimataifa katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo na kulinda usalama na maendeleo ya kikanda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |