Wadau wa soka Tanzania wamelipokea kwa furaha wazo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kuwa kama hali itaendelea kama ilivyo basi ataruhusu michezo na vyuo kufunguliwa kwa wiki inayoanzia Jumatatu. Afisa habari wa shirikisho la soka Tanzania TFF Cliford Mario Ndimbo, afisa habari wa Simba SC Haji Manara na afisa mhamasishaji mkuu wa Yanga SC Antonio Nugaz wameeleza kufurahishwa na wazo hilo, hiyo ikiwa inatoa mwanga kwao wa kurejea kwa Ligi hivi karibuni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |