Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga nchini Tanzania, Dk. Mshindo Msolla amezindua kampeni ya kuelekea mfumo wa mabadiliko ya kiuendeshaji kwa klabu hiyo kongwe. Dk. Msolla amesema kamati ya mabadiliko itakuwa chini ya kamati ndogo itakayosimamiwa na Mwanasheria Alex Mgongolwa huku mchakato wote wa mabadiliko ya kimfumo ukisimamiwa na kufadhiliwa na mdhamini mkuu wa klabu hiyo GSM ukiwa na kaulimbiu 'TWenzetu kwenye Mabadiliko'. Yanga inataka kubadilika na kuwafuata watani zao wa jadi Simba ambao tayari wameanza mfumo mpya wa uendeshaji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |