• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) watoa wito kwa wafanyabiashara kuzingatia vipimo sahihi

    (GMT+08:00) 2020-05-21 19:33:40
    Mkurugenzi wa ufundi Wakala wa Vipimo (WMA) nchini Tanzania ,Stella Kahwa ,amewataka wanunuzi na wauzaji kuzingatia matumizi sahihi ya vipimo katika biashara ili kuweza kufikia uchumi wa kati.

    Kahwa aliyasema hayo jana katika maadhimisho ya siku ya Vipimo Duniani ambayo hufanyika Mei 20 kila mwaka huk kauli mbiu ya mwaka huu ikiwa ni "Vipimo katika Biashara za Kimataifa".

    Bi Kahwa alisema kuwa nchi ya viwanda inajengwa kwa kuzingatia vipimo sahihi kwa kuangalia malighafi mpaka mali inayozalishwa.

    Aidha Kahwa aliishukuru serikali ya Tanzania kwa kuwawezesha kwa kiasi kikubwa kwani mpaka sasa wana magari ya kutosha ,watumishi wameongezwa ,pia wamefanikiwa kupata kituo kikubwa kwa ajili ya kupimia magari ya mafuta.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako