Wanasoka wanane kutoka timu maarufu nchini Mexico Santos Laguna wamekutwa na maambukizi ya virusi vya Corona, hivyo kuweka kikwazo kwa kuanza tena kwa Ligi ya taifa iliyosimamishwa kwa miezi miwili. Ligi hiyo ilitarajiwa kuanza tena mwishoni mwa wiki, na matokeo ya vipimo hivyo yanaleta ugumu zaidi katika nia ya kurejesha michuano hiyo. Mpaka sasa ni majibu ya vipimo 22 kati ya 48 vya wachezaji na makocha ndio yaliyotolewa. Mmiliku wa timu hiyo Alejandro Irarragorri amesema, wachezaji hao wanane waliokutwa na maambukizi ya virusi vya Corona, hawakuwa na dalili zozote za virusi hivyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |