Mkutano mkuu wa mwaka wa baraza la mashauriano ya kisiasa la taifa umefanyika hapa Beijing. Rais Xi Jinping wa China ameshiriki kwenye kikao cha wajumbe wa sekta ya uchumi wa baraza hilo.
Rais Xi amesema China inatakiwa kuchukulia kukidhi mahitaji ya ndani kuwa msingi wa maendeleo, kuharakisha kujenga mfumo kamili wa mahitaji ya ndani, kuhimiza uvumbuzi na kuharakisha shughuli mpya za kimkakati zinazojitokeza, ukiwemo uchumi wa kidigitali na uzalishaji kwa kutimia akili bandia na kuunda nguvu nyingi zaidi zinazohimiza ukuaji mpya.
Rais Xi amesema hivi sasa uendeshaji wa uchumi wa China unakabiliwa na shinikizo kubwa, inatakiwa kujipatia maendeleo katika dunia inayokumbwa na hali isiyo tulivu na yenye sintofahamu, lakini sifa ya kuwa na uwezo mkubwa na fursa nyingi ya uchumi wa China haijabadilika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |