Akihutubia taifa kupitia taarifa iliyopeperushwa moja kwa moja kutoka Ikulu ya Nairobi mnamo Jumamosi, Mei 23, 2020, kiongozi wa taifa amesema wakati umewadia kwa taifa kurejelea maisha ya kawaida sawa na baadhi ya mataifa mengine duniani.
Rais ameeleza kwamba itakuwa muhimu Kenya kufungua tena shughuli zake za kiuchumi akifafanua kwamba taifa haliwezi kusalia katika hali ya kufungwa.
Hata hivyo, ametahadharisha kwamba ili kufanikisha hatua hiyo, zitahitajika juhudi za kila Mkenya binafsi katika kuzingatia masharti yaliyotolewa na Wizara ya Afya.
Amewahimiza Wakenya kufuata masharti na kanuni za Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya janga la virusi vya corona pamoja na kuwalinda Wakenya wenzao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |