• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Huenda shughuli za kiuchumi zikafunguliwa kote nchini bila zuio na kafyu

    (GMT+08:00) 2020-05-25 15:43:09
    Wakenya huenda wakarejelea maisha yao ya kawaida kipindi cha majuma machache yajayo pasipo kafyu na zuio la kuingia au kutoka katika baadhi ya kaunti, endapo kauli ya Rais Uhuru Kenyatta ni ya kuzingatiwa.

    Akihutubia taifa kupitia taarifa iliyopeperushwa moja kwa moja kutoka Ikulu ya Nairobi mnamo Jumamosi, Mei 23, 2020, kiongozi wa taifa amesema wakati umewadia kwa taifa kurejelea maisha ya kawaida sawa na baadhi ya mataifa mengine duniani.

    Rais ameeleza kwamba itakuwa muhimu Kenya kufungua tena shughuli zake za kiuchumi akifafanua kwamba taifa haliwezi kusalia katika hali ya kufungwa.

    Hata hivyo, ametahadharisha kwamba ili kufanikisha hatua hiyo, zitahitajika juhudi za kila Mkenya binafsi katika kuzingatia masharti yaliyotolewa na Wizara ya Afya.

    Amewahimiza Wakenya kufuata masharti na kanuni za Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya janga la virusi vya corona pamoja na kuwalinda Wakenya wenzao.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako