• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Watalii wamininika nchini

    (GMT+08:00) 2020-05-25 15:43:25
    Siku chache baada ya tangazo a rais John Magufuli kwamba atafungua anga za Tanzania kwa usafiri wa ndege za kimataifa, tayari watalii wameanza kuwasili nchini humo. Ndege ya kwanza iliwasili wiki jana na kutua katika uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro. Miongoni mwa abiria saba waliotua, wanne kati yao ni watalii kutoka Ugiriki.

    Alhamisi wiki hii, Tanzania inatarajia kupokea ndege nyingi zaidi zikiwamo za watalii. Awali, Rais Magufuli alidokeza kwamba, watanzania watarajie watalii wengi kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni.

    Tayari mashirika kadhaa ya ndege yameratibiwa safari za kusafirisha vyakula na mizigo mingine kutoka Tanzania hadi mataifa mengine.

    Aprili, 11, mwaka huu, Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Tanzania (TCAA), yalifuta safari zote za ndege za abiria kutokana na mlipuko wa virusi vya corona.

    Hata hivyo, kutokana na tathmini ya mwenendo wa virusi hivi, Mei 18 mwaka huu, serikali ya Tanzania ilitangaza kufunguliwa kwa usafiri wa anga ya Tanzania kwa ndege zote za kibiashara, misaada, kidiplomasia, za dharura na ndege maalum.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako