Goli la mshambuliaji wa klabu ya Aston Villa ya Uingereza Mbwana Samatta aliloifunga Liverpool kwenye michuano ya UEFA Champions League November 5 2019 dhidi ya Liverpool limeandika historia. Samatta akiichezea KRC Genk ya Ubelgiji wakati huo goli lake alilowafunga Liverpool ndio limetajwa na ukurasa rasmi wa Genk kama ndio goli bora la mwaka la klabu hiyo. Katika mchezo huo uliomalizika kwa KRC Genk kupoteza kwa kufungwa magoli 2-1, Samatta alifunga goli maridhawa la kichwa dakika ya 41. Hata hivyo Samatta aliondoka KRC Genk mwezi Januari 2020 na kujiunga na Aston Villa ya Uingereza kwa kiasi kinachotajwa kufikia pound milioni 10 akisaini mkataba wa miaka minne na nusu kusalia Villa Park.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |