Klabu ya Olympic Lyon ya Ufaransa imeripotiwa kuanza ushindani wa kisheria na Shirikisho la soka Ufaransa (FFF) kufuatia uamuzi wao wa kumaliza msimu 2019/20 na kuitangaza PSG kama Bingwa. Lyon watapeleka kesi hiyo katika Mahakama za juu za Ufaransa, ikizingatiwa msimu huo umemalizika na msimamo kutambulika wao wakiwa nafasi ya 7 hivyo wanakosa hata nafasi ya kucheza Europa League. Ligue 1 na Ligue 2 Ufaransa zilimalizwa April huku Legue 1 ikiwa zimesalia mechi 10 kumalizia msimu kitu ambacho Lyon kinawaumiza na kulalamika kuwa klabu zitapoteza mapato ya karibia euro milioni 900. Rais wa klabu ya Lyon Jean-Michel Aulas ndio anaongoza malalamiko hayo na tayari ameshaongea na mamlaka husika akipeleka malalamiko yao Mahakamani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |