Shirikisho la Riadha nchini Kenya (AK) linapanga kufanya mikutano kadhaa kuanzia mwishoni mwa mwezi Agosti ili kujiandaa na mashindano ya Kip Keino, moja ya mashindano ya riadha duniani yanayotarajiwa kufanyika Septemba 26 jijini Nairobi. Rais wa Shirikisho hilo Jackson Tuwei amesema kama serikali italegeza vizuizi vilivyowekwa kudhibiti kuenea kwa virusi vya Corona, kuna uwezekano wa kufanya mashindano ya kaunti nay a kikanda kabla ya mashindano ya kitaifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |