Watu kumi wameuawa na wengine sita walijeruhiwa jana Jumapili baada ya basi dogo walilokuwa wakisafiria kukanyaga bomu lililotegwa kando ya barabara pembezoni mwa Mogadishu, Somalia.
Msemaji wa serikali ya Somalia Bw. Ismael Mukhtar Omar amethibitisha kutokea kwa mlipuko huo kwenye barabara kati ya Mogadishu na Afgoye jana asubuhi.
Mpaka sasa hakuna kundi lolote lililotangaza kuwajibika na shambulizi hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |