• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wakenya wanaendelea kuumia kutokana na bei ya juu ya bidhaa badala ya kupata afueni iliyotarajiwa baada ya kupungua kwa bei ya mafuta

    (GMT+08:00) 2020-06-02 19:50:24

    KWA kipindi cha miezi miwili sasa, Wakenya wamekuwa wakinunua mafuta kwa bei ya chini kuliko ilivyo kawaida.

    Kwa mfano, mwezi uliopita, Mamlaka ya Kawi na Mafuta (EPRA) ilitangaza punguzo la karibu Sh10 na Sh20 kwa kila lita ya mafuta ya petroli na dizeli mtawalia.

    Ongezeko la bei ya mafuta limekuwa likitumiwa kama kigezo cha kuongeza bei ya bidhaa muhimu kama vile vyakula, maji na umeme.

    Ripoti kuhusu bei ya bidhaa iliyotolewa wiki iliyopita na Shirika la Takwimu (KNBS), inaonyesha kuwa bei ya bidhaa muhimu iliongezeka kwa kiasi kikubwa kati ya Aprili na Mei mwaka huu.

    Bei ya vyakula kama vile sukumawiki, maharagwe, spinachi, machungwa, karoti, vitunguu na vinywaji visivyokuwa na vileo nayo imekuwa ikiongezeka kwa kasi tangu Aprili, kwa mujibu wa ripoti ya KNBS.

    Wataalamu wa masuala ya uchumi walikuwa wametabiri kuwa kupungua kwa bei ya mafuta kungepunguza gharama ya uzalishaji na usafirishaji wa bidhaa, hivyo kuwapa Wakenya afueni.

    Jambo la kushangaza ni kwamba Wakenya wanaendelea kuumia kutokana na bei ya juu ya bidhaa badala ya kupata afueni iliyotarajiwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako