Kituo cha Kukinga na Kudhibiti Magonjwa cha Afrika, (Africa CDC) kimesema, idadi ya kesi za maambukizi ya virusi vya Corona barani Afrika imefikia 152,442.
Kituo hicho kimesema, idadi hiyo imeongezeka kwa kesi 5,343 kutoka 147, 99 ya jumatatu, na idadi ya vifo pia imeongeza na kufikia 4,344.
CDC pia imesema, virusi hivyo vimeenea katika nchi 54 za Afrika, na nchi zilizoathiriwa zaidi ni Afrika Kusini, Misri, Nigeria, Algeria, Ghana na Morocco.
Jumla ya watu 63,661 wamepona virusi hivyo barani humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |