Hatimaye Kocha wa Klabu ya Azam FC, Aristica Cioaba amerejea nchini Tanzania kuendelea na kibarua chake kuifundisha timu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara, huku pia akiwahi mechi ya robo fainali ya Kombe la FA kati ya timu yake dhidi ya SImba itakayopigwa Juni 27. Cioaba aliwasili Tanzania jumatatu jioni pamoja na kocha wa viungo, Costel Birsan wakitokea Frankfurt, Ujerumani ambako ndiko walipata usafiri wa ndege ya kurejea Tanzania, na walitarajiwa kuanza kazi jana jioni huku kikosi hicho kikiwa tayari kimeanza mazoezi chini ya kocha msaidizi, Bahati Vivier.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |