Wanamgambo wasiopungua 18 kutoka kundi la CODECO wameuawa na jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kwenye operesheni iliyoanza Jumatatu kwenye eneo la Djugu mkoani Ituri, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Msemaji wa kikosi cha DRC kwenye eneo hilo Luteni Jules Ngongo, amesema lengo la operesheni hiyo ni kuwazuia wanamgambo hao kushambulia raia na polisi kwenye eneo hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |