Waziri mkuu wa Palestina Bw. Mohammed Ishtaye ameonya kuwa Palestina itaacha kuitambua Israel kama serikali yake itatekeleza mpango wake wa kukalia ardhi ya Palestina.
Bw. Ishtaye amesema ukaliaji wa Israel kwenye maeneo ya uUkingo wa Magharibi, hasa Bonde la Jordan, unalenga kuhujumu uwezekano wa kuanzisha nchi huru ya Palestina.
Waziri mkuu huyo pia amethibitisha kuwa upande wa Palestina umesitisha kikamilifu uratibu wote na Israel kwenye nyanja za uchumi, afya na usalama.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |