Tume ya Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM imekiri kuwa raia watatu waliuawa na wengine wawili walijeruhiwa kwenye mapigano yaliyotokea Jumatatu kati ya vikosi vya tume hiyo na wapiganaji wa Al-Shabaab kusini mwa Somalia.
Mkuu wa AMISOM Bw. Francisco Madeira amesema tukio hilo limetokea wakati magaidi wa al-Shabaab walipofanya shambulizi la ghafla katika njia kuu ya ugavi kwenye eneo la kaskazini mashariki mwa Janaale mkoani Lower Shabelle.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |