• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Watu 81 wauawa na wanaoshukiwa kuwa ni wapiganaji wa Boko Haram Nigeria

    (GMT+08:00) 2020-06-11 09:08:08

    Watu wasiopungua 81 wameuawa na wengine saba wametekwa nyara wakati watu wanaoshukiwa kuwa ni wapiganaji wa Boko Haram waliposhambulia kijiji kimoja katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa Nigeria.

    Gavana wa jimbo la Borno Bw. Babagana Zulum amesema watu wengine 13 wamejeruhiwa na wapiganaji hao ambao walishambulia kijiji cha Faduma Koloram kwenye eneo la Gubio mapema Jumanne.

    Gavana huyo amesema shambulizi hilo ni la tatu dhidi ya kijiji hicho ndani ya mwezi mmoja, na serikali itaendelea kuunga mkono vikosi vya usalama kuhakikisha usalama wa maisha na mali za watu wa huko.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako