China imetoa msaada ya dawa za kemikali na vifaa kwa Uganda ili kupambana na nzige wanaoathiri usalama wa chakula wa nchi hiyo.
Balozi wa China nchini Uganda amesema msaada huo ni sehemu ya ushirikiano wa kilimo kati ya nchi hizo mbili. Msaada huo wa tani 20 utasaidia kuongeza jitihada za Uganda kupunguza athari ya uvamizi wa nzige.
Kwa upande wake waziri wa kilimo wa Uganda Bw. Vincent Ssempijja ameishukuru China kwa msaada huo, na kusema itatoa mchango kuhakikisha usalama wa chakula nchini humo. Habari zinasema Uganda imefanya maandalizi kukabiliana na nzige ambao wamesababisha hasara kubwa kwa nchi jirani Kenya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |