Kituo cha Sayansi ya Mifumo na Uhandisi cha Chuo Kikuu cha Johns Hopkins cha Marekani, kimesema, hadi kufikia saa tano dakika 33 usiku kwa saa za huko, idadi ya maambukizi ya virusi vya Corona nchini Marekani imefikia 2,000,464, huku watu 112,924 wakifariki.
Jimbo la New York bado ni eneo linaloathiriwa zaidi likiripoti kesi 380,156 za maambukizi na vifo 30,542. Majimbo mengine yenye wagonjwa zaidi ya laki 1 ni pamoja na New Jersey, California, Illinois na Massachusetts.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |