Kampuni ya Dongfang Electric ya China (DEC) imesema imesaini makubaliano na muungano wa kampuni mbili za Misri kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa kituo kikubwa cha umeme wa maji nchini Tanzania.
Kwa mujibu wa makubaliano, kampuni ya DEC itatoa mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia nishati ya maji na vifaa husika kwa mradi wa kituo cha umeme wa maji cha Julius Nyerere kwenye bonde la mto Rufiji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |