Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametuma salamu za rambirambi kwa wananchi wa Burundi kufuatia kifo cha rais wa nchi hiyo, Pierre Nkurunziza.
Taarifa iliyotolewa na serikali ya Burundi imesema, Rais nkurunziza alifariki Jumatatu kutokana na mshtuko wa moyo katika hospitali moja mjini Bujumbura.
Nkurunziza alichaguliwa kuwa rais wa Burundi mwaka 2005 na alichaguliwa tena katika chaguzi za mwaka 2010 na 2015. Alikuwa amekabidhi madaraka kwa rais mpya mwezi Agosti baada ya uchaguzi uliofanyika nchini humo Mei 20.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |