Kenya inakaribia kufikia kilele cha maambukizi ya virusi vya Corona, wakati ikikabiliwa na shinikizo la mfumo wa afya ambao umekumbwa na mzigo mkubwa wa maambukizi ya magonjwa mengine nchini humo.
Katibu mkuu wa wizara ya afya ya Kenya Dkt Rashid Aman amsema kuwa takwimu za hivi karibuni za maambukizi mapya ya virusi vya Corona ni ushahidi wazi kwamba nchi hiyo inakiribia kufika kileleni, hivyo kuna haja ya kuimarisha hatua za kuzuia na kuepusha mlipuko mkubwa unaoweza kuzidi uwezo wa miundombinu ya huduma za Afya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |