Umoja wa Mataifa umethibitisha kutokea kwa matukio zaidi ya elfu 25 ya udhalilishaji mkubwa wa watoto kwenye mapigano ya kisilaha yaliyotokea mwaka 2019. Kwa mujibu wa Ripoti ya mwaka ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu watoto na mapigano ya kisilaha iliyotolewa jana jumatatu, mwaka jana watoto 10,173 waliuawa au kulemazwa, na Afghanistan bado ni nchi yenye hatari kubwa zaidi kwa watoto ikifuatiwa na Syria na Yemen. Ripoti pia imesema watoto 7,747, baadhi yao wakiwa na umri wa miaka sita, walitumikishwa kwenye mapambano mwaka jana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |