Rais mteule wa Burundi Evariste Ndayishimiye anatarajiwa kuapishwa Alhamisi wiki hii kufuatia mahakama ya kikatiba ya nchi hiyo kutoa uamuzi wiki iliyopita kuwa atashika wadhifa wa urais baada ya rais Pierre Nkurunziza kufariki dunia. Wizara ya mambo ya nje ya Burundi jana jumatatu ilitoa mwaliko kwa wanadiplomasia wa nchi za nje nchini humo kuhudhuria sherehe ya kuapishwa itakayofanyika Juni 18 katika mkoa wa kati wa Gitega.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |