Sudan imetangaza kuwa inapinga hatua ya upande mmoja ya kujaza maji kwenye bwawa kubwa la Ethiopia GERD lililoko kwenye mto Nile bila makubaliano kufikiwa kati ya Sudan, Misri na Ethiopia.
Waziri wa maji na umwagiliaji wa Sudan Bw. Yasir Abbas amesisitiza haki ya nchi zote kupata mgao sawa wa raslimali za maji bila kuleta uharibifu. Waziri huyo pia ameyataja mazingira ya mazungumzo kuwa ni "mazuri" kwa ajili ya kufikia makubaliano kabla ya Julai mosi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |