Kuwait imeamua kulegeza hatua za karantini zilizochukuliwa kuzuia kuenea kwa virusi vya Corona kuanzia wiki ijayo.
Msemaji wa serikali ya Kuwait Tareq Al-Mezrem amewaambia wanahabari kuwa zuio jipya la kutoka nje litatekelezwa kutoka saa usiku hadi saa 11 asubuhi kuanzia Juni 21. Aidha, serikali ya nchi hiyo imeamua kuondoa zuio la usafiri kwenye maeneo ya Hawally, Nuqra, Maidan Hawally na kuondoa baadhi ya vizuizi kwenye eneo la Khaitan kuanzia Jumapili ijayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |