Hadi kufikia jana Alhamisi, wafanyakazi wapatato 730 katika machinjio ya jimbo la North Rhine-Westphalia (NRW) nchini Ujerumani wamethibitika kuambukizwa virusi vya Corona baada ya kupimwa.
Mamlaka za huko zimeamuru kufunguwa kwa kiwanda cha kuchakata nyama cha Kundi la Toennies kwenye eneo la Guetersloh jimboni humo kuanzia jumatano. Aidha, watu wapatao 7,000 wamewekwa karantini kwenye eneo la Guetersloh. Jimbo la NRW limeanzisha uchunguzi kuhusu chanzo cha maambukizi hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |