Shirikisho kuula Wafanyabiashara wa Afrika mkoani Guangdong, China limefanya mkutano na matawi yake wakati wa maonyesho ya 127 ya biashara ya Guangdong yaliyoanza jumatatu wiki hii kwa njia ya mtandao wa Internet, na kusema litawahimiza wafanyabiashara wa Afrika washiriki kwenye maonesho hayo.
Wajumbe wa Shirikisho hilo wameeleza imani yao kuhusu maonyesho hayo na ushirikiano wa biashara kati ya China na Afrika, na kusema wanapenda kusukuma mbele kwa pamoja utekelezaji wa biashara ya mtandao kwenye maonyesho hayo.
Shirikisho hilo limesema, maonyeshao hayo yanatoa fursa kwa makampuni ya Afrika kuona na kuagiza bidhaa, na kutembelea viwanda vya kuzalisha bidhaa hizo kupitia mtandao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |