Benki kuu ya Brazil imesema wachambuzi wa masuala ya uchumi wa Brazil wamekadiria kuwa Pato la Ndani la Taifa GDP la nchi hiyo litapungua kwa asilimia 6.5 mwaka huu, baada ya kuendelea kushuka kwa wiki 18 mfululizo.
Kwa mujibu wa Ripoti ya wiki hii ya benki hiyo, ukuaji wa uchumi wa Brazil kwa mwaka kesho unakadiriwa kuwa asilimia 3.5.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |