Tetemeko la ardhi lenye nguvu ya 7.5 kwenye kipimo cha Richter limetikisa jimbo la Oaxaca kusini mwa Mexico, na mpaka sasa limesababisha kifo cha mtu mmoja.
Tetemeko hilo lililotokea saa 4 na dakika 29 jana asubuhi limeharibu baadhi ya majengo na miundombinu ya mawasiliano, na kusababisha maporomoko ya udongo.
Rais Andrés Manuel López Obrador wa Mexico siku hiyo amesema serikali kuu imedumisha mawasiliano ya karibu na serikali ya jimbo hilo, ili kufahamu zaidi hali ya janga hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |