Wizara ya Afya nchini Rwanda imezindua mpango wa kuwapima virusi vya Corona wazee wenye umri wa zaidi ya miaka 60 na watu wenye magonjwa sugu kama kisukari na magonjwa ya mfumo wa hewa katika wilaya ya Rusizi magharibi mwa nchi hiyo.
Eneo hilo ambalo liko katika mpaka kati ya Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ni moja ya maeneo matatu nchini Rwanda ambayo yameripoti kesi mpya za virusi hivyo, na sehemu ya wilaya hiyo imefungwa kuanzia tarehe 4 mwezi huu.
Wizara ya afya imeweka maabara ya kufanyia vipimo katika wilaya ya Rusizi ili kuhakikisha majibu ya haraka ya vipimo hivyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |