• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Umoja wa Ulaya wapanga kufungua upya mipaka kwa baadhi ya nchi

    (GMT+08:00) 2020-06-24 16:23:38

    Nchi nyingi za Umoja wa Ulaya zimepunguza udhibiti wa maeneo ya mipaka, na kuanzia tarehe Mosi mwezi ujao, Umoja huo utafungua mipaka yake kwa baadhi ya wasafiri wa nje isipokuwa wanaotoka Marekani.

    Hivi sasa, maofisa wa Umoja huo wanajadiliana kuhusu usalama wa wasafiri wanaoingia kutoka nje. Pia Umoja huo umesema, hautaruhusu watu kutoka Marekani kuingia katika nchi wanachama wa Umoja huo kutokana na idadi kubwa ya vifo vinavyotokana na maambukizi ya virusi vya Corona nchini Marekani.

    Watu kutoka Brazil, Mexico na India pia huenda wakazuiliwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako