Waziri wa afya wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Eteni Longondo leo ametangaza kuwa, maambukizi ya virusi vya Ebola katika sehemu ya kaskazini mashariki mwa nchi hiyo yametokomezwa.
Kwa mujibu wa waziri huyo, tangu maambukizi ya Ebola yatokee nchini humo mwezi Agosti mwaka 2018, DRC imeripoti kesi za jumla 3,470 za maambukizi ya virusi vya Ebola, na watu 2,287 kati yao wamekufa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |