Viongozi wa sekta ya uzalishaji kutoka Kenya na Misri wamesema baadhi ya nchi za Afrika zimeanza kushuhudia kufufuka polepole kwa biashara baada ya miongozo mipya ya kupambana na virusi vya Corona kuanza kutekelezwa.
Ofisa mkuu mtendaji wa Jumuiya ya wazalishaji viwandani ya Kenya Bibi Phyllis Wakiaga, amesema kuna dalili za kufufuka kwa uzalishaji baada ya serikali na sekta binafsi kuanza kununua bidhaa zilizotengeneza ndani.
Kiongozi wa mfuko wa kupambana na COVID-19 wa Kenya Bw. James Mwangi, amesema baadhi ya viwanda vya kuzalisha vifaa vya kujikinga (PPE) vimeanza kuwaita
Mwenyekiti wa bodi ya chama cha wenye viwanda vya kemikali nchini Misri Bw. Sherif El Gabaly amesema kuna ongezeko la usafirishaji nje kutoka Misri, na hii ni kutokana na kuwa na msingi mzuri wa viwanda na kilimo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |