Zaidi ya wataalam 10 wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wamesema, uamuzi wa serikali ya Marekani ya kuweka vikwazo dhidi ya wafanyakazi wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Kijinai (ICC) ni shambulizi la moja kwa moja kwa uhuru wa kisheria wa mahakama hiyo, na unaweza kudhoofisha waathirika kupata haki. Juni 11 Rais Donald Trump wa Marekani alitoa amri ya kuzuia mali za wafanyakazi kadhaa wa ICC.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |