Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limesema wahamiaji haramu 71, wameokolewa katika pwani ya Libya. Wahamiaji hao pamoja na wanawake wanne na watoto wawili, wamepelekwa katika mji mkuu wa Libya Tripoli na walinzi wa pwani. Tangu kupinduliwa kwa kiongozi wa zamani marehemu Muammar Gaddafi mwaka 2011, Libya imekuwa kituo kinachopendelewa na maelfu ya wahamiaji haramu kuvuka bahari ya Mediterranean na kwenda Ulaya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |