Takwimu zilizokusanywa na Chuo Kikuu cha Johns Hopkins cha Marekani zinaonyesha kuwa, hadi kufikia jana, idadi ya watu waliofariki kutokana na virusi vya Corona imezidi laki 5 duniani, na watu walioambukizwa virusi hivyo wamezidi milioni 10. Marekani inaongoza kwa kuwa na idadi kubwa zaidi ya maambukizi na vifo. Nchi nyingine zenye idadi ya vifo zaidi ya elfu 20 ni pamoja na Brazil, Uingereza, Italia, Ufaransa, Hispania na Mexico.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |