Serikali ya Afghanistan imesema, wapiganaji 64 wa kundi la Taliban wameuawa katika operesheni ya siku mbili iliyofanywa na jeshi la Afghanistan katika sehemu mbalimbali nchini humo.
Kundi la Taliban la nchini Afghanistan lilitangaza kusimamisha vita kwa siku 3 kabla ya sikukuu ya Idi el Fitr. Baada ya sikukuu hiyo, kundi hilo liliendelea kushambulia vikosi vya jeshi la serikali, ambalo pia liliongeza nguvu ya kujibu mashambulizi hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |