Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema yuko tayari kufanya mazungumzo na uongozi wa Palestina kwa msingi wa mpango wa amani wa Mashariki ya Kati uliotolewa na rais Donald Trump wa Marekani. Vyombo vya habari vya Israel Ijumaa iliyopita vilimnukuu ofisa mwandamizi wa Palestina akisema, Israel ilimwarifu rais Mahmoud Abbas wa Palestina kuwa, itapunguza kwa kiasi kikubwa maeneo yanayokaliwa nayo kando ya Magharibi ya Mto Jordan.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |