Naibu katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Rosemary DiCarlo amesema makubaliano ya nyuklia ya Iran na azimio namba 2231 la Umoja wa Mataifa yana umuhimu mkubwa kwa kuzuia usambazaji wa silaha za nyuklia na usalama wa kikanda na kimataifa. Akitoa taarifa kuhusu utekelezaji wa azimio hilo kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Bi DiCarlo pia alieleza kusikitishwa na hatua ya Marekani ya kujiondoa kwenye makubaliano, na kwa Iran kusimamisha utekelezaji wa vipengele kadhaa vya makubaliano hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |